TyDiQA1.0

The Typologically Different Question Answering Dataset

Predictions

Scores

Kalamashaka

The Typologically Different Question Answering Dataset

Kalamashaka (kwa jina lingine K-Shaka) ni kundi la hip hop lenye makao yake katika mtaa wa Dandora, kitongoji katika mji wa Nairobi, Kenya. Kinajumuisha wasanii watatu: Oteraw, Kama na Johny. Kikundi hiki kiliundwa katika miaka ya katikati ya 1990. Walikuwa maarufu kwa wimbo wao Tafsiri Hii uliovuma sana mwaka wa 1997. Kundi hili lilifungua pazia kwa wasanii nyota kadhaa wa kimataifa kati yao Coolio na Lost Boyz na wameimba pamoja na Dead Prez na wasanii wengine wa kimataifa. Wametumbuiza katika nchi kadhaa kama vile Nigeria, Uswidi, Uholanzi, Afrika Kusini, Norway miongoni mwa nyingine. Kalamashaka walifungua njia kwa hip hop katika lugha ya Kiswahili na ikawa inatawala nchini Kenya. Kikundi hiki ni maarufu na mashabiki wake kwa muziki wake wa hardcore rap na wenye ujumbe wa kijamii na kisiasa. Albamu yao ya kwanza Ni Wakati iliyotolewa mwaka wa 2001 ilivuma sana na Channel O ya Afrika Kusini ilicheza mmoja ya video "Fanya Mambo" kutoka katika albamu hii. Albamu hii iliangazia uhalifu mitaani, ukabila, siasa na migogoro ya Afrika. Umaarufu wao ulianza kupungua wakati mitindo ya Genge na Kapuka ilipoibuka ambayo ilikuwa inaweza kuchezeka kwa urahisi na yenye tasfoa ambayo asilimia kubwa ya vijana wanapendelea kusikiliza kuliko muziki wa kifalsafa. Stesheni za redio za FM husita kucheza miziki yenye mpigo wa kijamii kama unaochezwa na Kalamashaka na kupelekea kupungua kwa umaarufu wao. Hata hivyo, kikundi hiki kimeendelea kufanya kazi na kukataa kubadili mtindo kulingana na nyakati na kufanya biashara ya muzik. Kundi hili lilisukuma makundi mengine kama Mashifta, Gidi Gidi Maji Maji, K-South, Necessary Noize na wasanii wengine wengi. 

Je,kundi la Kalamashaka ilianza mwaka upi?

  • Ground Truth Answers: 1990miaka ya katikati ya 19901990

  • Prediction: