Walimwengu ni jina la wimbo uliotoka 2007 kutoka kwa msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka nchini Tanzania, Nuru the Light. Katika wimbo, Nuru ameangalia sana tabia za kibinadamu ambazo rahisi kutokea. Namna watu wanavyokupenda ukiwa na kitu halafu kukubadilikia ukiwa huna kitu. Hali ambayo inatokea kila siku katika jamii yetu. Hii ni kazi ya SoulHouse Studio, huku video ikiwa kazi ya Adam Juma kupitia Visual Lab.