Madume wana pembe nyeusi mbili zenye umbo la pia zitokazo kichwa kwa kukaribiana tu nyuma ya macho. Pembe hizo huendelea juu, lakini hupinda mbele kidogo; zina urefu wa sm 15–24 kwa nilgai mzima. Ingawa kwa kawaida pembe hizo ni laini, pembe za madume wazee zaidi zinaweza kuwa na migongo ya duara karibu na tako lao.[1]