Casablanca ina bandari kubwa ya Moroko[1] ikiwa ni pia kitovu cha benki kubwa za nchi hii. Kufuatana na sensa ya 2012 idadi ya wakazi ilizidi milioni nne katika wilaya yake. Hivyo inatazamiwa kama mji mkuu wa kiuchumi ilhali mji mkuu wa kisiasa ni Rabat.